BARNABA AWAJIA JUU WANAOMTUKANA KWA KUVAA SKETI

MUZIKI ni biashara, lakini kuna
watu hawajui. Mwimbaji mwenye sauti tamu masikioni, Barnaba, hivi majuzi
aliachia picha akiwa amevaa nguo za kike, akidai ni biashara.
Lakini baadhi ya mashabiki, bila
kujali kauli hiyo wamemvaa na kumpa maneno yasiyo na staha.
"Sijali watu wote wanaonitukana,
kuna watu wenye heshima zao wamenipongeza kwa sababu wanajua ni biashara, na
siyo kuvaa tu ili mradi," anasema msanii huyo ambaye pia anajulikana kama
Mopao.
"Wanaokereka wataendelea
kukereka maana Septemba hii nitavaa kila aina ya nguo za kike kama sketi,
madera, vijora na nimeshatoa tenda kwa madesigners wangu Wolperstylish kunishonea
nguo nyingi za kike," anasema Barnabaclassic.

Post a Comment