MICHEZO YOTE MIWILI YA AWALI AZAM FC KUCHEZEA NYUMBANI

 Inaweza kuwa picha ya Watu 9, watu wanasimama na nyasi

 

AZAM FC ambayo itashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika Msimu huu, itaanza hatua ya awali kwa kucheza mechi zake zote mbili nyumbani.

Azam imethibitisha kuwa michezo yote miwili ya hatua ya awali ya kombe la shirikisho Afrika (Caf Confederation Cup preliminary Round ) dhidi ya Horseed FC ya Somalia itachezwa Tanzania.

Mchezo wa kwanza Azam FC watakuwa nyumbani mchezo utachezwa Chamanzi kwenye uwanja wao wa Azam Complex na mchezo wa marejeano timu ya Horseed FC itakuwa mwenyeji na mchezo wake utachezwa katika uwanja wa Uhuru Stadium(zamani shamba la bibi)

 

No comments