LICHA YA JESHI KUONDOKA, MAREKANI ITAENDELEA KUHAMISHA RAIA WAKE

 Marekani yasema Urusi ilituma ndege za kijeshi Libya | Matukio ya Afrika |  DW | 26.05.2020

 

 

MAREKANI imesema itaendelea na zoezi la kuwahamisha Wamarekani zaidi kutoka nchini Afghanistan licha ya Jeshi la Marekani kuondoka kabisa nchini humo jana Jumatatu ambapo Mshauri wa usalama wa kitaifa wa Marekani Jake Sullivan kama aliyosema Rais Biden, amesema zoezi la uokoaji ndilo lililobadilika kutoka oparasheni za moja kwa moja za kijeshi hadi oparasheni za kidiplomasia.

Amesema Marekani ina makubaliano na Taliban juu ya kuwaruhusu Wamarekani waliosalia Afghanistan kuondoka Nchini humo idadi ambayo ni chini ya Watu 200 na kusisitiza kwamba Marekani itaendelea kutuma misaada ya chakula, matibabu na aina nyengine ya misaada ya kibinadamu kwa Waafghani.

Hata hivyo amesema misaada mengine ikiwa ni pamoja ya kiuchumi na maendeleo itategemea vitendo vya Taliban kama watatekeleza ahadi walizozitoa kwa umma baada ya kuingia madarakani. 

 

 

No comments