RC MAKALA APOKEA KERO 91 ZIARANI DAR

 Breaking News: RAIS MAGUFULI AMTUMBUA MKUU WA MKOA WA KATAVI AMOS MAKALA. -  YouTube

KATIKA ziara ya Kibamba, RC Makalla amesema jumla ya kero 96 amezipokea kwa njia ya maandishi na zote zimepitiwa moja baada ya nyingine ili kuhakikisha wananchi hao wanapatiwa haki zao kwa wakati huku nyingi zikiwa ni migogoro ya ardhi kutoka katika Kata ya Kwembe.

Hata hivyo amewataka watendaji wote aliowapa maagizo wakati wa kutatua kero hizo, watekeleze maagizo hayo, nakuwa kinyume na hapo ni kupuuza maelekezo ya yake.

"Migogoro mingi ya ardhi inaonekana kuwepo Kata ya Kwembe, hivyo nakuaguza Kamishana wa ardhi uyashughilikie na watu wapate majibu.

Leo Septemba 1, 2021 RC Makalla ataendelea na ziara ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika jimbo la Segerea, viwanja vya Buguruni Vijana.

No comments