KAMPENI YA CHANJO SASA HADI VIJIJINI

 Samia Suluhu Hassan | Habari za UN

WAKATI serikali ikiendelea kuhamasisha wananchi kupata chanjo ya ugonjwa wa corona hasa sehemu za mijini, kampeni kubwa inayofanyika sasa ni kupeleka chanjo vijijini ili Watanzania wengi waweze kuipata.

Msemaji mkuu wa serikali, Gerson Msigwa amesema mwishoni mwa mwezi Septemba au mwanzoni mwa Oktoba 2021 kutakuwa na “Wiki ya Uchanjaji” ambapo viongozi nchi nzima watashiriki moja kwa moja kwenye wiki hiyo kuhakikisha watanzania wengi wanapata chanjo ili kuepuka madhara ya ugonjwa huo.

 

No comments