EWURA YASHUSHA BEI YA MAFUTA ILIYOPANDISHWA JANA


 EWURA YADHIBITI UCHAKACHUAJI MAFUTA KUTOKA 80% HADI 4%, MATUMIZI GESI  ASILIA YAFIKIA TANI 189,509

KAIMU Mkurugenzi wa EWURA, Godfrey Chibulunje leo, Septemba 1, 2021 ametangaza kuwa bei ya mafuta iliyotolewa jana imebadilika na bei itakayotumika ni ileile iliyokuwa ikitumika mpaka kufikia jana Agosti 31, 2021.

“Jana tulitangaza bei mpya ya mafuta ambayo ilitakiwa ianze kutumika leo Septemba 1, lakini sasa bei hizo zimeoneka zikiendelea kupanda na hata kwenye soko la dunia kwa sababu zingine ambazo zipo inaoneka bei inaendelea kuwa kubwa.

“Kwa mantiki hiyo sasa tumepata maelekezo mahususi kutoka Serikalini kwamba bei hizo zisitishwe na bei ziendelee kutumika zilezile zilizokuwa zikitumia mpaka kufikia siku ya jana.

“Tume maalum imeundwa kuchunguza na kuangalia mwenendo mzima wa upandaji wa bei,” Amesema Chibulunje.

 

No comments