BORA TUFIE HUKU AFGHANISTAN KULIKO KUREJEA NYUMBANI UGANDA

NI KAMA kituko ila ndiyo ukweli. Licha ya ukweli
kwamba wanamgambo wa Taliban wanaotawala Afghanistan kwa sasa ni tishio hata
kwa wananchi wao wenyewe, raia wa Uganda walioko huko wamekataa ofa ya serikali
kuwarejesha nyumbani.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda, Jenerali Jeje
Odongo amesema Waganda walioko Afghanistan wamegoma kurudi Uganda
Jen. Odongo amesema kati Waganda walioko Afghanistan ni
watatu tu walioko tayari kurudi na wameshaandaliwa utaratibu huku wengine
wakisema wako salama.
Nchi kadhaa zimekuwa zikiwatoa raia wake baada ya Taliban
kudhibiti nchi.

Post a Comment