TSHABALALA AONGOZA KWA FOLLOWERS INSTA!

 Inaweza kuwa picha ya Mtu 1

 

NAHODHA Msaidizi wa Simba, Mohammed Hussein 'Zimbwe Junior' maarufu zaidi nchini kama Tshabalala, ndiye mwanasoka mwenye wafuasi wengi zaidi katika mtandao wa Instagram kuliko wengine wote.

 

Siri hiyo imefichuliwa na Kaimu Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, akisema wakati duniani yupo mshambuliaji nyota Cristiano Ronaldo, hapa nchini tunaye Tshabalala.

 

"Kule Cristiano, huku Tshabalala

Kwa taarifa tu; nahodha msaidizi wa Simba SC Tanzania Mohamed Hussein "Zimbwe Jr" ndiye msakata ndinga anayecheza Tanzania mwenye wafuasi wengi zaidi hapa Instagram. Sasa kafikisha followers 893,000. Namba moja nchi nzima kwa wanasoka.

Ni matarajio yangu kampuni na wadhamini wanaona takwimu kama hizi. Manchester leo wanaringa kumpata Cristiano Ronaldo kwa sababu wafuasi wake Insta - nazungumzia watu milioni 333, sasa wataanza kufuatilia habari za Man Utd.

Fursa ndiyo hii. Na kapteni wangu huyu hana baya. Hana kashfa. Hana ukorofi. Mtu muungwana. Ni faida kwa brand yoyote. Mtazameni kwa jicho la biashara!!!

 

No comments