NEC YATANGAZA UCHAGUZI MDOGO KONDE, USHETU


MKURUGENZI NEC AWAJIBU CHADEMA... - Uzalendo wa Kitanzania | Facebook

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema Uchaguzi Mdogo katika Majimbo ya Konde (Mkoa wa Kaskazini Pemba) na Ushetu (Shinyanga) utafanyika Oktoba 09, 2021

Wagombea watachukua fomu kuanzia 13-19 Septemba, uteuzi utafanyika Septemba 19 na Kampeni zitaanza 20 Septemba hadi 08 Oktoba.

Jimbo la Konde lipo wazi baada ya Mbunge Mteule kujiuzulu na aliyekuwa Mbunge wa Ushetu na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa , Elias John Kwandikwa kufariki dunia Agosti 02 mwaka huu.

No comments