MZEE ALIYEMBAKA HOUSEGIRL KORTINI JUMANNE 31 AGOSTI 2021

MSHTAKIWA Sadalla Juma Sadalla mwenye umri wa miaka 74 mkazi wa Bububu, Unguja,
atafikishwa mahakamani Vuga, Jumanne 31 Agosti 2021 kwa makosa ya kumbaka
msichana wake wa kazi mwenye umri wa miaka 15 (jina limeifadhiwa).
Mshitakiwa Sadalla Juma Sadalla
alifikishwa mahakamani mara ya kwanza Agosti 18, 2021 na kusomewa mashataka
yake na kesi hiyo imepangiwa tena tarehe 31 Agosti 2021 katika mahakama ya Vuga
mjini Unguja. Katika juhudi la kukomesha vitendo vya ubakaji na udhalalishaji
visiwani Zanzibar, serikali ya mapinduzi ya Zanzibar na vyombo vya ulinzi
vinajitahidi kuwafikisha mbele ya sheria wale wote watakaotenda makosa hayo ya
ubakaji na udhalalishaji.
Mshitakiwa Sadalla Juma Sadalla alilalamikiwa na wanaharakati visiwani Zanzibar
kuwa ni mzoefu katika vitendo vya ubakaji pamoja na udhalalishaji na alipombaka
msichana wake wa kazi mwenye umri wa miaka 15, alikuwa yupo huru na alipanga
kuondoka unguja kukimbia kesi hiyo baadhi ya majirani zake walisika lakini
vyombo vya usalama viliwahi kumshika na hatimaye kumpeleka
mahakamani.Mshitakiwa Sadalla Juma Sadalla yupo mahabusu kwa kuwa shitaka la
kubaka, udhalalishaji halina dhamana.

Post a Comment