MCHUNGAJI, MKEWE WAFUNGWA MIEZI 18

 Ahukumiwa maisha jela kwa kumpa mimba mwanaye | East Africa Television


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Bukoba imewahukumu Merchades Mugishagwe anayejiita Mtumishi wa Mungu kifungo cha miezi 18 na faini ya shilingi million 3 na Mkewe Agripina Pius kutumia kifungo cha nje kwa muda huo wa miezi 6 baada ya mahakama hiyo kuwatia hatiani kwa kushindwa kutimiza majukumu yao kama wazazi.

Watu hao wawili walikuwa wanakabiliwa na mashitaka 8 yakiwemo ya kushindwa kutimiza wajibu wao kama wazazi na kutowapeleka watoto wao watatu shule waliokuwa wametimiza umri wa kwenda shule kwa madai ya kuwa Mungu wa Isaka na Yakobo hatambui elimu ya dunia.

No comments