ASKARI WALIOUAWA DAR WAAGWA

 IMG_0067.jpg


WAOMBOLEZAJI mbalimbali leo wameshiriki katika hafla ya kuwaaga askari polisi wanne waliouawa kwa kupigwa risasi katika uwanja wa Kambi ya Polisi, Kilwa Road ilipo Hospitali ya Polisi.

Askari hao waliuawa Agosti 25, 2021 katika majibizano ya risasi katika eneo la Oysterbay, Barabara ya Ali Hassan Mwinyi, jijini Dar es Salaam.

Miili ya askari hao inaagwa leo Agosti 27, 2021 huku Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Simon Sirro akiongoza zoezi hilo.

No comments