MBUNGE CCM AMCHARUKIA GWAJIMA

KUFUATIA mzozo kati ya Bunge na Mbunge wa Kawe kupitia CCM, Askofu
Josephat Gwajima juu ya chanjo ya corona, mwakilishi wa wananchi kutoka
Singida, Elibariki Kingu amekuja na maneno haya....
"Hichi anachokifanya Gwajima ni
kiburi kilichojaa kuvimba na kulewa sifa za dunia na si sifa za kuwakilisha
Mungu katika madhabahu.
"Askofu Gwajima ametoa tuhuma nzito kwa nchi, na mimi
nimejiuliza maswali hivi ni kweli jeshi la polisi halioni
"criminality" iliyopo katika kauli za Gwajima, hivi kweli jeshi la
Polisi halioni hatari ya kauli za Gwajima kwamba zinaweza zikasababisha Serikali
ikapinduliwa kwamba Rais ameamua kuuza watu wake.
"Adhabu zitakazotolewa kwa Askofu Gwajima kwa hili
zisiishie hapo, hata huyu aliyekuwa Mbunge wa Kawe, Halima Mdee hajawahi
kutufanyia vitimbi vya namna hii, nshangaa sana kwanini Chama changu kimekaa kimya
mpaka sasa.
"Rais Magufuli kama Mungu angekuwa amemtunza hai mpaka
leo, Gwajima angeweza kufungua mdomo wake na kuleta hizi chokochoko, kama kuna
mbunge anafikiri kwamba atatumia "forum" hii kwa sababu tu
hakupendezwa na Rais Samia kuwa madarakani, Wallahi nakuambia tutadili
nae,akitokea mmoja akataka kujenga umaarufu binafsi badala ya umaarufu wa
taasisis na kulinda mifumo ya Taifa letu, kabla ya kuja kwako Spika,
tutatwangana makonde huko."

Post a Comment