MBATIA ALISHUKIA JESHI LA POLISI

 72D3A426-3714-46AB-B4ED-3FFE0BB5328F.jpeg


 

MUDA mchache baada ya chama chake cha NCCR-Mageuzi kuzuiwa kufanya mkutano wake wa ndani na Jeshi la Polisi, Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, James Mbatia, amelishukia kwa maneno makali jeshi hilo lililo chini ya IGP, Simon Sirro.

 

"Hata kama watatuua sote hatuwezi kukubali serikali inavyondeshwa kibabe bila kufuata Katiba, kila mtu kambale mamba masharubu tu hatuwezi kuendelea na mambo ya ajabu ajabu kama haya, kwanini hata kauli ya Amir Jeshi Mkuu haiheshimiwi!?? Tanzania tunaenda wapi??.

"Nasema kwa dhati kabisa kwamba hawa wanaozuia mikutano ya vyama vya Upinzani wanachochea chuki na wanachochea hasira kwa Watanzania nyie ndio Magaidi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania msiwasingizie wengine.

"Jeshi la Polisi mimi ni M/kiti wa Chama cha Siasa Tanzania nani asiyenijua nawasiliana na IGP hajibu simu yangu, nawasiliana na RPC hawajibu simu zangu, nyie ndio mnapandikiza chuki na mnaihujumu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"Nchi imekuwa ya hovyo kabisa, Polisi mmeota masharubu mmeshindwa hata kuheshimu kauli ya Rais kwamba vyama vinaruhusiwa kufanya mikutano ya ndani sasa ni kauli ya nani itaheshimiwa katika nchi hii?? Sisi tuna hasira kweli kweli Rais tunakuomba tuzungumze mdharau mwiba mguu huota Tende.

"Kama Jeshi la Polisi mmeamua kulianzisha sisi NCCR-Mageuzi tunaweza kulimalizia, tumefanya siasa za kuunganisha nchi na kutafuta maridhiano kwa muda mrefu ili kuisaidia nchi yetu ila mmeendelea kutuona wajinga mmekosa uungwana mnataka kulivuruga Taifa hili, sisi tupo tayari kwa lolote kuanzia sasa tumechoka kunyanyasika ndani ya Nchi yetu wenyewe.

"Nchi imejaa chuki, angalia mauaji aliyofanya Kijana Hamza watu wanashangilia hii inaonesha dalili ya chuki kwa Taifa, tunatoa pole kwa Familia za Marehemu wote ikiwapo Familia ya Hamza kwa kuwa na yeye ni binadamu na tunawapa pole chama cha Mapinduzi kwa kuondokewa na kada wao Hamza ni kada wao wasikatae sisi NCCR-Mageuzi tunawapa pole.


 

 

No comments