MAPATO BANDARI TANZANIA YAONGEZEKA

LICHA ya janga la ugonjwa wa Corona
linaloisumbua dunia, bandari za Tanzania zimerekodi ongezeko la mapato kwa
miezi sita kutoka shilingi bilioni 525.4
hadi shilingi Bilioni 531.
Msemaji Mkuu wa serikali, Gerson
Msingwa amesema, mapato haya si haba, kwenye kipindi cha Covid-19 zipo bandari
nchi za wenzetu wamerekodi 0% ya mapato, Bandari zetu zimeendelea kufanya
vizuri licha ya changamoto za Ugonjwa wa Uviko-19 Duniani”.
“Bandari yetu imeboreshwa kina kimechimbwa zaidi ili Meli
kubwa zaidi ziweze kufika, kutokana na uwezekazaji huu Bandari yetu ya Dar es
Salaam wiki tatu zilizopita imeandika rekodi kubwa kwa Bara la Afrika, ambapo
kupitia gati maalumu ilifanikiwa kupokea magari 3743, na asilimia 65 ya magari
hayo (magari 2945) yalikuwa yanapelekewa nje ya Nchi, mapato yameongezeka"——— @gersonmsigwa
“Sasa nitakuwa nazungumza na Watanzania kila kiki Kwa taarifa
fupifupi, teknolojia inaturuhusu sitowalazimisha waandishi kuja kwenye mkutano
tutawaletea taarifa kwenye vyumba vyenu vya habari, itakuwa ni taarifa fupifupi
na Watanzania watapata nafasi ya kuuliza maswali hata leo hapa baada ya maswali
ya waandishi tutapokea maswali ya Wananchi Kwa njia ya simu”

Post a Comment