KAULI YA SIRRO KWA WAZAZI WA HAMZA ZAKOSOLEWA

 Sirro apangua makamanda, ateua RPC mpya Dar - Mwananchi

KAULI ya Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Simon Sirro juu ya kuwataka wazazi kutozaa watoto wa hovyo kama walivyo wazazi wa Hamza Mohammed, kijana aliyewaua polisi wanne kabla ya yeye kuuawa na polisi, imekosolewa na wadau mbalimbali nchini.

Hamza, kada wa CCM na ambaye chanzo cha tukio lake bado hakijawekwa wazi na Polisi ambao bado wapo katika uchunguzi, aliwaua polisi hao siku chache zilizopita, akipambana nao kwa zaidi ya dakika 45.

Sirro, akizungumza katika siku ya kuwaaga polisi waliouawa, alisema kijana Hamza ni matokeo ya wazazi kuzaa watoto hovyo, hivyo akawataka wazazi wengine kutokuwa kama wa Hamza.

Hata hivyo, makundi ya wadau mbalimbali, wamemkosoa kiongozi huyo mkuu wa Jeshi la Polisi, wakidai maneno yake hayakuwa sawa, kwani hakuna mzazi, akiwemo yeye, anayeweza kujua tabia zijazo za mtoto wake.

No comments