DUCHU, AME WATOLEWA KWA MKOPO SIMBA

KLABU ya Simba imethibitisha
kuwatoa kwa mkopo walinzi wake wawili vijana waliokosa nafasi katika kikosi cha
kwanza.
Hao ni mlinzi wa kati Ibrahim
Ame, aliyesajiliwa kutoka Coastal Union ya Tanga msimu uliopita ambaye amepelekewa
Mtibwa Sugar na mlinzi wa pembeni kulia, David Kameta maarufu kama Duchu ambaye
atakuwa na klabu ya Biashara United ya Mara ambayo pia itashiriki michuano ya
kombe la Shirikisho msimu huu.

Post a Comment