BIMA YA AFYA KWA WOTE YATENGEWA FEDHA

 ZanziNews : NHIF Yatajwa Kuchangia Mageuzi Sekta ya Afya Miaka Minne ya JPM

SERIKALI kupitia kwa msemaji wake imeeleza kuanza kutekeleza Sheria ya Bima ya Afya kwa wote, ambapo imetenga Fedha Shilingi Bilioni 149 kwa ajili ya mpango huo.

Msemaji wa Serikali Gerson Msigwa ametoa kauli hiyo mjini Dodoma katika mkutano wa Sita uliowakutanisha Wahariri wa vyombo vya habari na mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.

Amesema mpango huo utatekelezwa baada ya muswada wake kufikishwa bungeni mwezi Septemba mwaka huu ili kuwa Sheria rasmi na kuanza kutumika, ambapo utaanza kwa kuwasaidia wananchi wasiokuwa na uwezo wa kulipia gharama za matibabu.

Kwa Upande wake Mkurugenzi mkuu wa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bernard Konga, amesema yapata miaka 20 tangu kuanzishwa kwa mfuko huo ambao umewezesha kuboresha Sekta ya Afya kwenye Hospitali kubwa hapa nchini pamoja na vituo mbalimbali vya Afya.

No comments