UBAGUZI WAONDOA UHAI WA KINDA WA SOKA ITALIA

UBAGUZI wa rangi..Tabia ya wazungu kuwabagua waafrika umeendelea na safari hii umeshindwa kuhimili uvumilivu kwa kijana Seid Visin kuamua kujiua baada ya kudhalilishwa kila kona akiwa nchini Italia.
Seid Vision amewahi kuichezea timu ya vijana ya
AC Milan.
Kabla ya kuamua kujitoa roho, mwanasoka huyo
aliyekufa akiwa na umri wa miaka 20 tu aliandika;
"Sikuja nchini Italia kwa kupenda bali nilichukuliwa
kutoka nyumbani Ethiopia na wazazi wawili wa Kiitaliano (Adoption) wakanileta
huku kama mtoto wao.
"Mwanzoni maisha nchini Italia yalikuwa mazuri na kila mtu
alinipenda ila mambo yalianza kubadilika punde baada ya kupata ajira ya kufanya
kazi hotelini.
"Wateja walisusia huduma yangu, wengi niliowahudumia
walinifukuza kama Mbwa, huko viwanjani pia kila siku ilikuwa ni ubaguzi dhidi
ya rangi yangu na Uafrika wangu.
"Nilitengwa kila sehemu, haswa watoto wa Kiitaliano
ambao hawana kazi ila mimi sikuwahi kuchagua kazi, hivyo nimeamua kukatisha
maisha yangu kwa kuwa sina wa kumlilia wala wa kunisaidia."

Post a Comment