MWIZI MSANII HATIMAYE ADAKWA


Inaweza kuwa picha ya maandishi yanayosema 'DUNIA INA MAMBO Mwizi ambaye amekuwa akijifanya mzimu akiwatisha wakaazi wa Gutu, Jimbo la Masvingo nchini Zimbawe hatimaye amekamatwa. Mwizi huyo anadaiwa kuvunja maduka na nyumba za watu huku akiwa amevalia mavazi ya mzimu wa Halloween. Wenye mali walikuwa wakimwona, walikuwa wanakimbia kwa hofu wakiamini wameona mzuka wa kweli kumbe ni mwizi amekuja kama mzımu anaboa na kuiba vyote.'

 KILA kazi ili ufanikiwe, ni lazima uwe mbunifu, utofautiane na wengine.

Ndivyo ilivyokuwa kwa mwizi huyu wa kuvunja na kubomoa nyumba, huko Gutu katika Jimbo la Masvingo nchini Zimbabwe.

Inadaiwa kuwa mwizi huyo alikuwa akivaa mavazi yanayofanana na mizimu ya Haloween na akijitokeza, kwa hofu wenye nyumba hukimbia wakiamini wamekutana na mzuka wa kweli.

Huku nyuma, mwizi huyo huchukua vitu vyote anavyovihitaji na kutoweka. Baada ya muda mrefu, wakazi hao wakakata shauri na kumwekea mtego uliomnasa kirahisi.

No comments