SIKIA TAMBO ZA JOSEPH MBILINYI 2PROUD A.K.A SUGU


Inaweza kuwa picha ya Watu 3 na maandishi yanayosema 'Sugu MikeT Dola Soul'

HAPANA shaka kwamba Joseph Mbilinyi ndiye staa wa kwanza wa Hip Hop Tanzania, kwani tangu achomoze mwishoni mwa miaka ya 1990, heshima yake haijashuka hadi leo.

Katika mitandao mbalimbali ya kijamii, leo zimepostiwa picha zake akiwa na wakali wenzie enzi hizo, Mike Mnyalu 'Mike T' na Balozi Dola Soul.

Lakini Sugu hakuacha tabia zake za kihp hop, za matambo juu ya matambo. Msikie akiizungumzia picha hiyo ya mwanzoni mwa miaka ile ya 2000.

"Angalia katika vidole vyangu, angalia shingoni na ile saa niliyovaa mkononi. Na bado nje nimepaki ndinga."

No comments