MAGEREZA WAKANUSHA OLE SABAYA KUGOMA KUOGA


Sabaya afikishwa Mahakamani Arusha – Millardayo.com

 KUKIWA na taarifa kwamba aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya anayeshtakiwa kwa makosa sita ya uhalifu kugoma kuoga mara baada ya kutinga mahabusu gerezani, Mkuu wa Magereza Mkoani Arusha, Godson Mwanagwa amekanusha taarifa hizo.

"Alipokelewa vizuri tu hakuna vurugu zilizotokea, hakuna tukio kama hilo lililotokea, aliyetoa taarifa mngemuambia amezitoa wapi, Mimi mhusika nakuambia wanaoripoti ni waongo," alisema Godson Mwanangwa.

Kesi ya Sabaya imekuwa gumzo kubwa nchini, wananchi kutoka pande zote wakiwa na maoni tofauti. Sabaya atasubiri mahabusu katika kipindi chote cha kesi yake kwa vile baadhi ya makosa anayotuhumiwa nayo hayana dhamana.

No comments