DOLA BILIONI 30 KULALA MRADI GESI ASILIA LINDI


Wakazi 120 kufaidika na gesi asilia

WAKATI Serikali ikihaha huku na kule kuhakikisha Tanzania inakula jasho kutokana na rasilimali zake, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali ipo mbioni kuanza kutekeleza mradi wa kimkakati wa uzalishaji wa gesi asilia ya kimiminika (LNG) mkoani Lindi utakaogharimu dola za kimarekani bilioni 30.

Amesema kuwa Mradi huo ni moja ya mradi wa kimkakati ambao Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amepania kuutekeleza katika awamu ya sita ambao utakapoanza kutekelezwa itatumika kwa kipindi cha zaidi ya miaka 25.

Ametoa kauli hiyo leo Jumamosi Juni 5, 2021 wakati wa mkutano na wadau wa maendeleo wa Wilaya ya Lindi, katika ukumbi wa hoteli ya Sea View Mjini Lindi.

"Vile viwanja mlivyovichukua anzeni kuvijenga, mradi wa gesi asilia unakuja, nina amini mradi huu ukianza baada ya kukamilisha makubaliano, tutafika hatua nzuri."


No comments