GRUPU LA WHATSAPP LACHANGIA MIFUKO 300 YA SIMENTI NACHINGWEA BOYS HIGH SCHOOL

HAYA ndiyo mambo sasa. Badala ya kutumia magrupu ya whatsApp kwa mambo yasiyo ya msingi, wananchi wa Wilaya ya Nachingwea kupitia grupu lao la Nachingwea yetu, wamejichanga na kununua mifuko 300 ya simenti kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo.
Baadhi ya wananchi wa Nachingwea
ambao wapo ktk kundi sogozi la WhatsApp la NACHINGWEA YETU, wamekabidhi mifuko
300 ya saruji kuunga mkono ujenzi wa mradi mpya wa Nachingwea Boys High School inayojengwa kwa kutumia
mapato ya ndani ya halmashauri ya wilaya ya Nachingwea iliyopo mkoa wa Lindi
Shule hiyo inatarajiwa kukamilika kwake kuchukua wanafunzi
1600 kuanzia kidato Cha Kwanza Hadi Cha sita.
Aidha shule hiyo mpya ya wavulana inatarajiwa kuwa na jumla
ya majengo 54 ikiwemo madarasa, mabweni, nyumba za walimu, duka, zahanati na
sehemu ya kula chakula.
Shule hiyo inajengwa nje kidogo ya mji wa Nachingwea katika Kijiji
cha Chiumbati Kata ya Chiumbati Tarafa ya Naipanga.
Akizungumza wakati wa kupokea mchango huo, aliyekuwa
Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo ambaye kwa sasa ni Katibu Tawala mkoa wa DSM, Hassan
Abasi Rugwa, amewashukuru wadau hao wa Nachingwea Yetu Whatsapp group kwa
mchango wao na kuwasisitiza wananchi wa Nachingwea kuendelea kushikamana kwa
pamoja ili kufanya Mambo makubwa zaidi.
Serikali imeonesha nia ya kuunga mkono ujenzi wa shule hiyo
baada ya kuona jitihada za dhati zinazofanywa na wananchi.

Post a Comment