BANANGA ATOFAUTIANA NA LISU KUHUSU DIAMOND


Ally Bananga on Twitter: "Kupumzika siku 3 kwa @TunduALissu kufanya  kampeni, Naanza kuona CCM wananenepa . Just wait for 4 the return  #Maji_wataita_mma… https://t.co/m7q7RYKe8r"

WAKATI Tundu Lissu akitaka wapenda demokrasia wasimpigie kura za kushinda Tuzo za BET msanii Diamond Platnums, mwanachama mwenzake wa Chadema, Binamu Bananga, amesema yeye ni shabiki wa kijana huyo wa Tandale na kwa hiyo atampigia kura.

Katika kushibisha hoja yake, Bananga amesema pamoja na tofauti za kiitikadi zilizopo baina yao, linapokuja suala la michezo, muziki na starehe, hivyo ni vitu havina itikadi.

"Mimi ni shabiki wa Diamond, lazima nitampigia kura, siwezi kuacha kuishabikia Simba kwa sababu mfadhili wake Mo ni mtu wa CCM. Huwa nachagua vita ya kupigana, vita ndogo vina gharama kubwa kama hupigani kwa tahadhari.

"Siyo lazima nile kware wakati nina kuku. Wajibu wangu kisiasa ni mkubwa kuliko kumuombea mabaya mtanzania anayejiinua, kama humuungi mkono waachie wanaomuunga."

No comments