WAZIRI UMMY MWALIMU ATEMA NYONGO SOKONI KARIAKOO


ITV Tanzania - Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu ametangaza... | Facebook

 WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa (TAMISEMI), Ummy Mwalimu leo alitembelea soko Kuu la Kariakoo na kuzungumza na wafanyabiashara. Hii hapa ripoti yake kwa wananchi kupitia mtandao wake wa kijamii.

"Jana tar 22/5/2021 nilifanya ziara Sokoni Kariakoo kufuatilia jumbe nyingi za simu nilizopokea kutoka kwa wafanyabiashara wa Soko hili. Baada ya kuwasikiliza wafanyabiashara wa Soko la Kariakoo nakiri pasi na shaka kuwa lipo tatizo ambalo tunapaswa kulitatua haraka ili kurudisha Hadhi na Heshma ya Soko la Kariakoo.

"Tuhuma na kero za wafanyabiashara nilizopokea ni pamoja na mfanyabiashara kudaiwa rushwa ya hadi shilingi milioni 4 ili aweze kukodishwa kizimba/kigoli, kodi kubwa ya shilingi laki 7 kwa mwezi kwa wapangaji wa vigoli vya nje ya soko halafu mbele kuna mpangaji tena anaeuza bidhaa hizohizo akilipa kodi ya shilingi 51,000 kwa mwezi.

"Uwepo wa tozo kubwa kwa wafanyabiadhara wa meza, kutoruhusiwa magari ya karoti na mbogamboa kushusha mizigo sokoni Kariakoo kama ilivyokuwa zamani, uwepo wa madalali wa vigoli pamoja na uwepo wa ubadhilifu wa fedha za mali za Shirika la Masoko ya Kariakoo.

"Ili kutatua kero hizi, nimeamua kuunda Kamati huru ya kuchunguza tuhuma hizi na kuniletea Taarifa ndani ya siku 14.

"Nitoe rai kwa wafanyabiashara wa sokoni Kariakoo kuendelea kuwa watulivu na kufanya biashara zao kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu. 
#KaziIendelee

No comments