ROMA MKATOLIKI AKOSA USHAWISHI KWA DEMU WAKE KUHUSU SIMBA KUTOLEWA CAF CHAMPIONS LEAGUE

MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya maarufu kama Bongo Fleva, Roma Mkatoliki, amekiri kwamba ni ngumu sana kumfahamisha mwanamke wake kuwa timu anayoishabikia ya Simba, imeshinda, lakini imetolewa katika mashindano.
Kwenye akaunti yake
kunako mitandao ya kijamii, Roma Mkatoliki ameandika: Hamna kazi ngumu kama
kumuelewesha demu kuwa tumeshinda aafu tumetolewa.
Hapa alikua
anamaanisha licha ya ushindi mzuri wa Simba wa mabao 3-0 dhidi ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini
katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika, Simba haikufuzu hatua ya
nusu fainali kwani katika mchezo wa kwanza kule Johannesburg, wekundu hao wa
Msimbazi, walipigwa 4-0.

Post a Comment