WATANI SASA DIMBANI JULAI 3 KWA MKAPA

 Tanzania Football Federation - Wikipedia

MCHEZO wa Ligi Kuu Tanzania Bara ulioahirishwa katika mazingira ya kutatanisha Mei 8 mwaka huu, sasa utapigwa Julai 3 ndani ya Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara, mchezo huo ambao umeshaahirishwa mara mbili huko nyuma, utapigwa saa 11 jioni, kama ambavyo ilikuwa imepangwa awali katika mchezo wa Mei 8, 2021.

 

No comments