WALIOPITA HAPA HAWAKURUDI KUSIMULIA

 President Obama Looks Out the "Door of no Return" | The White House

KWA kawaida, binadamu tunafanya mambo mengi katika maisha yetu kabla ya kufa. Baadhi ya tunayofanya, hutupa burudani na mafunzo pia kwa wenzetu.

Mathalan, yapo mambo ambayo tunapoyapitia, tunapata pia muda wa kuwasimulia wengine ili nao wafurahi, waguswe au hata wajiandae kukabiliana nayo pindi yakiwakuta.

Lakini kwa Kisiwa cha Goree, kilichopo katika jiji la Dakar, kule nchini Senegal ni tofauti kwa miaka ile mingi iliyopita.

Wakati ule mchafu wa biashara ya watumwa, katika kisiwa hicho, kulikuwa na jengo maalum la kusubiria abiria wakati meli, mashua, au boti zikitia nanga. Wazungu walilijenga jengo hilo na kuuweka mlango ambao ulipata umaarufu mkubwa kwa jina la A Door Of No Return wakimaanisha, ukipita katika mlango huo, hautarudi tena ulikotoka.

Mamia kwa maelfu ya watumwa kutoka nchi za Afrika Magharibi walipitia mlango huu na kupelekwa Ulaya na Marekani kwenda kufanya kazi katika mashamba na viwandani. Wengi pia walioumwa au kuleta ubishi, walitoswa baharini na kufa.

Rais Barak Obama wa Marekani wakati wa ziara yake barani Afrika, alifika katika nchi hiyo na kutembelea lango hilo. Aliposimuliwa kilichotokea, alitoa machozi kwa uchungu.

 

No comments