BARAKOA: VAZI RASMI IKULU, MITAANI HAWALIJUI

WAKATI Rais Samia
Suluhu Hassan akionyesha kwa vitendo juu ya hofu yake kwa ugonjwa wa Covid 19,
Watanzania wengi bado hawaamini kama nchi yao siyo kisiwa, hivyo wanaendelea
kujiachia bila tahadhari juu ya janga hilo la kidunia.
Shughuli zote za
kiserikali hivi sasa zinaendana na vazi la barakoa, linalozuia maambukizi ya
ugonjwa huo, lakini mitaani ni kama vile watu hawajui lolote juu ya Covid 19
kwani, kuvaa barakoa ni gharama isiyo na sababu.
Ndani ya mabasi ya
abiria maarufu kama daladala, watu wanaendelea kujazana bila tahadhari yoyote
kuchukuliwa, katika maeneo ya soko, stendi, misibani, harusi na kote huko,
mambo ni kama kawaida, kuvaa barakoa ni kupenda mwenyewe.
Kama serikali
imetambua uwepo wa ugonjwa huu, ni budi kuchukua hatua za makusudi, kulazimisha
taifa zima kutambua janga hili. Daladala ziwe levo siti, maji tiririka yawepo
kila sehemu na umbali kati ya mtu na mtu katika shughuli za kijamii izingatiwe.

Post a Comment