TRA YAITIKIA WITO WA MAMA SAMIA

WIKI chache tu baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kutaka serikali kutotumia nguvu katika kudai kodi kwa wafanyabiashara, Mamlaka ya Mapato Nchini TRA, leo imetangaza kuzifungulia akaunti zote za wafanyabiashara zilizokuwa zimefungwa kwa kudaiwa kodi.
Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma wa
TRA, Richard Kayombo, alitoa msimamo huo mbele ya wahariri wa vyombo vya habari
wakati akitoa mada kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa Jukwaa la Wahariri TEF mjini
Morogoro leo.
"Si kawaida kushikilia akaunti ya
mfanyabiashara na uamuzi huu mara nyingi unakuwaga wa mwisho kabisa baada ya
jitihada zingine kushindikana ikiwemo majadiliano na mhusika," amesema
Kayombo.
"Tumeamua kuziachia hizi akaunti ili sasa
tuwe tunakaa mezani na kujadiliana na wafanyabiashara wenye madeni namna bora
ya kulipa taratibu taratibu na tunaachana na ule wa kushikilia akaunti
zao," alisema.

Post a Comment