WAKIMBIAJI 21 WAFA GHAFLA CHINA

 Rain, Hail, Ice, Sleet and Snow: Precipitation Matters to Organizational  Resilience | BOLDplanning Inc.

KUFUATIA hali ya hewa kubadilika ghafla, kutoka joto la kawaida hadi mvua ya mawe yenye baridi kali, wanariadha 21 wamepoteza maisha wakiwa mashindanoni (Ultramarathon) katika jimbo la Gansu, nchini China.
 
Maafisa wa eneo hilo wanasema mbio hizo zilizojumuisha Watu 172 ziliathiriwa ghafla na hali mbaya ya hewa ambapo ndani ya kipindi kifupi Joto lilipungua na kutokea mvua ya barafu.


Washiriki kadhaa walituma ujumbe wakiomba msaada na kufuatia hali kuendelea kuwa mbaya waandaaji waliahirisha mbio hizo na kutuma timu za waokoaji.

No comments