VILLARREAL MABINGWA EUROPA LEAGUE

TIMU ya Villarreal ya nchini Hispania imeibuka mabingwa wa michuano ya Europa League baada ya kuwafunga miamba toka England, Manchester United.
Katika mchezo huo wa fainali, wawili
hao walitoka sare ya bao moja kwa moja katika muda wa kawaida, Moreno
akiifungia Villarreal katika dakika ya 29, kabla ya Cavani kusawazisha dakika
ya 55.
Katika mikwaju ya penati, Villarreal
ilishinda 11 na Man United 10.
Hili ndilo Kombe lao Kubwa la kwanza
kuwahi kutwaa katika historia ya klabu hiyo.

Post a Comment