TWANGA PEPETA YAJA NA UZINDUZI, TUZO KWA MAGWIJI

 

Inaweza kuwa picha ya maandishi yanayosema 'TWANGA PEPETA ENTERTAINMENT PRESENTS TANZANIA MUSIC LEGENDS Concert TUZO ZA WANAMUZIKI MAGWIJI TANZANIA J'MOSI 29 MEI 2021 KIINGILIO: SH. 10,000 VIP SH. 20,000 BREAK POINT MAKUMBUSHO VILLAGE MORE TASTE MORE BITE sambamba na UZINDUZI wa albam ya TWANGA PEPETA BURUDANI: TWANGA PEPETA, MSONDO NGOMA, TUKUYU SOUND Tknyu Clouds THETEWITHIE HAIRUHUSIWI KUUZWAA +255 global GLOBALTV WASAFIFH KUSAMBAZWA KWA WALIO NA UMRI CHINI YA MIAKA 18. TAFADHALI KUNYWA KISTAARABU'

MIAKA nane sasa, bendi kongwe ya muziki wa dansi ya African Stars Twanga Pepeta haijatengeneza albamu, lakini mwishoni mwa mwezi huui, jambo hilo linakwenda kutokea pale Break Point, Makumbusho jijini Dar es Salaam.

Mara ya mwisho Twanga Pepeta ilitambulisha albam mpya "Usiyaogope Maisha" mwaka 2016 jijini Mwanza, wakati kwa upande wa Dar es Salaam tukio la aina hiyo lilifanyika 2013 kupitia albam ya "Nyumbani ni Nyumbani".

Katika uzinduzi wa albamu yake ya 14, Twanga itasindikizwa na Msondo Ngoma na Tukuyu Sound;

Albam ina jumla ya nyimbo sita: "Povu" utunzi wake Haji Ramadhani, "Twanga Mbele" uliotungwa na Kalala Jr ambaye kwasasa anaitumikia Tukuyu Sound, "Penzi Sigara Kali" ya Chaz Baba, "Ningekuwa" kutoka kwa chipukizi Joshua Pianno, "Rekebisha" na "Push to Start" zote za Said (Diouf) Msafiri.

 Boss wa Twanga Pepeta, Asha Baraka "Iron Lady" ameiambia Saluti5 kuwa jina la albam litatajwa ukumbini lakini akaongeza kuwa siku hiyo pia zitatolewa tuzo kwa wanamuziki wagwiji walioacha alama kwenye muziki wa dansi.

Twanga inajivunia muunganiko mzuri wa wapiga vyombo wanaofahamiana kwa muda mrefu na walioshikana ipasavyo wakiwemo Jojoo Jumanne (bass gitaa) Miraji Shakashia (solo na rythim gitaa), God Kanuti (solo na rythim gitaa), Victor Nkambi (Kinanda) na Kirukuu (drums).

Safu yao ya uimbaji inatisha kama njaa na imesheni mastaa tishio kwenye dansi kama vile Luizer Mbutu, Chaz Baba, Saleh Kupaza, Khalid Chokoraa, Msafiri Diouf na Haji Ramadhan bila kusahau vijana wawili wanaochipukia Joshua Piano na Tariq Zuberi ambao hakuna ubishi kuwa wameongeza ladha mpya kwenye bendi hiyo.

Ally Chocky 'Mzee Mbishi' amethibitisha atakuwepo katika onyesho hilo, uwepo ambao huenda ukajibu maswali mengi juu ya 'ndoa' tarajiwa kati yake na Twanga.

Credit: Salute5

 

No comments