VIJANA JKT WAITWA MAKAMBINI

TAARIFA KWA UMMA
WITO WA KURIPOTI
MAKAMBI YA JESHI LA KUJENGA TAIFA.
Mkuu wa Jeshi la Kujenga
Taifa (JKT), Meja Jenerali Charles Mbuge, anautaarifu Umma kuripoti makambini
Vijana waliochaguliwa kujiunga na Mafunzo ya JKT kwa Kujitolea kwa mwaka
2020/2021 ambao Mwezi Februari 2021 walirejeshwa majumbani.
Vijana wanaotakiwa
kuripoti makambi ya JKT waliyokuwa wamepangiwa hapo awali ni wale wenye Elimu
ya darasa la Saba na Elimu ya kidato cha nne. Waripoti makambini kuanzia tarehe
7 Mei hadi tarehe 14 Mei 2021.
Vijana wenye Elimu
ya Kidato cha Sita, Ngazi ya Cheti, Stashahada, Shahada na wale wenye Taaluma
ya Uhandisi wataendelea kusubiri majumbani hadi hapo utaratibu mwingine
utakapotangazwa.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Habari
na Uhusiano, Makao Makuu ya JKT,
Tarehe 30 April
2021.

Post a Comment