BASATA KUANZA KUWABANA WASANII LEO

LEO Mei 1 2021 ndio siku rasmi ambayo Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) linaanza kutumia kanuni ya kuzipitia nyimbo mpya za Wasanii wote Tanzania kabla ya kupelekwa kwenye Radio na televisheni.
“hii sio sheria mpya, ilikuwepo kabla ila
haikua imeanza kutekelezwa"
Naibu Katibu
Mtendaji wa BASATA Matiko S. Mniko amenukuliwa akisema;
"Kuanzia
tarehe 1 tutaanza kufanya oparesheni ya wale ambao hawafati utaratibu huu, kwa
sababu ya umuhimu wa utekelezaji wa kanuni hii, tuliunda kamati ambayo
imejipanga kwa ajili ya kuhakikisha kwamba kazi zote zinahakikiwa na hakuna
ambae atacheleweshewa"
"Kanuni hii
inataka Msanii kupeleka wimbo wake wa audio au video kwenye Baraza hilo kwa
ajili ya kupitiwa/kukaguliwa kwanza kabla ya kuuachia kwenye chombo chochote
cha habari, ukishakaguliwa na kupitishwa, BASATA itatoa cheti maalum cha
uthibitisho ambacho Msanii atatakiwa kwenda nancho kwenye Radio/TV na
kukionesha ili wimbo wake uanze kuchezwa."

Post a Comment