RAIS SAMIA ASUBIRIWA KWA HAMU NEEMA MEI MOSI LEO

 Samia Suluhu (@SuluhuSamia) | Twitter

LEO ni siku ya maadhimisho ya wafanyakazi duniani kote na kitaifa, sherehe hizo zinafanyika jijini Mwanza ambako mgeni rasmi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Maelfu ya wafanyakazi kote nchini, leo watakuwa wakimsubiri rais huyo wa kwanza mwanamke nchini, kutamka kile ambacho hawajawahi kukisikia kwa takribani miaka sita iliyopita, nacho ni nyongeza ya mishahara na upandaji madaraja.

Watumishi wa umma wameshindwa kupandishiwa mishahara na madaraja yao kwa kipindi chote cha serikali ya awamu ya Tano, iliyokuwa chini ya hayati Rais John Pombe Joseph Magufuli.

No comments