VIGOGO WIZARA YA FEDHA WAPIGWA CHINI KUPISHA UCHUNGUZI

MIEZI takribani miwili ikiwa imepita tangu Rais Samia Suluhu Hassan atoe agizo la kutaka Takukuru kufanya uchunguzi kuhusu fedha zote zilizotolewa Benki Kuu ya Tanzania kati ya Januari na Machi mwaka huu, vigogo kadhaa wamesimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi wa ukwapuaji wa mamilioni ya pesa katika Wizara ya Fedha.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
amewasimamisha kazi Mkaguzi Mkuu, Mkaguzi Msaidizi na baadhi ya Watendaji wa
Wizara ya Fedha. Amefanya hivyo ili kupisha Uchunguzi wa tuhuma za matumizi
mabaya ya Fedha za Umma.
Wakati akimuagiza Mkurugenzi wa Takukuru ACP Salum Hamduni
kufuatilia jambo hilo, Waziri Mkuu alisema fedha hizo zimetolewa kiutata,
zikitajwa kuwa ni malipo kwa kazi maalum ambazo hazikutajwa, malipo kwa kazi
ambazo ni majukumu ya kila siku ya watumishi hao, malipo ya siku ya Mei Mosi na
kadhalika.
Taarifa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu
iliyotolewa leo Mei 28, 2021 inaeleza kuwa katika kikao kazi na Waziri wa Fedha
na Mipango, Katibu Mkuu, manaibu katibu wakuu na watendaji waandamizi wa wizara
hiyo mkoani Dodoma jana, Majaliwa amemuagiza mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya
Kuzuia na kupambana na Rushwa (Takukuru), Salum Hamdun kufanya uchunguzi kuhusu
tuhuma hizo na ikithibitika si za kweli wahusika warejeshwe kazini.

Post a Comment