CHATO YAKATALIWA KUPEWA HADHI YA MKOA
IKIWA imepita miezi miwili tangu
wazee wa Chato kumuomba Rais Samia Suluhu Hassan kufikiria kuipa Chato hadhi ya
Mkoa, Baraza la Madiwani Geita limeukataa mpango huo na kuupinga kikaoni.
Rais Samia wakati akijibu ombi hilo katika hafla ya mazishi ya Rais John Magufuli iliyofanyika Chato, alisema atalifanyia kazi ikiwa ni pamoja na kuona kama vigezo vya kutangazwa kuwa mkoa vinakidhiwa.
Baraza Maalum la Madiwani Halmashauri ya Wilayani Geita Mkoa
wa Geita wamepinga wilaya mpya ya Busanda pamoja na hifadi ya Taifa ya Kisiwa
cha Rubondo kuchukuliwa na mkoa mpya wa Chato unaotarajiwa kuanzishwa wakidai
kuwa itasababisha wananchi kusafiri umbali wa kilomita 200 kwenda kutafuta
huduma na kusababisha mkoa wa Geita kukosa sifa kiutawala.
Madiwani hao wamesema baadhi ya maeneo yanayotakiwa
kuchukuliwa ili kwenda kujiunga na Chato kupata hadhi ya mkoa, kitaondoa sifa
za Geita kuwa Mkoa, jambo ambalo likifanyika halitakuwa na maana.

Post a Comment