TUMTUMIE DIAMOND KUTOBOA -PRODYUSA S2KIZZY


 SALMIN Kassim Maengo ambaye anafahamika zaidi kisanii kama s2kizzy amewataka watayarishaji wenzake wa muziki wa Bongo Flava, kumtumia nyota mkubwa Diamond Platnum katika kufikisha uwezo wao kimataifa, kwani ndiyo levo wanazozitafuta.

Prodyusa huyo ndiye anayefanya kazi ya kuandaa albamu mpya ya msanii huyo mwekezaji, ambayo inatakwa kuwashirikisha wasanii wakubwa kutoka kila pembe ya dunia. Na katika kuhakikisha kazi hiyo inafanyika katika viwango, S2kizzy amewaalika maprodyusa wengine nchini kujumuika naye kuingiza sound zao.

Kupitia The Switch, mtayarishaji huyo ambaye pia anafahamika kama Zombie alisema; ''Kwanza nashukuru kwakKuwa kwenye album ya Diamond, unaposhiriki kwenye album kubwa kama hii hata kama umefanya wimbo mmoja ni kitu kikubwa na unajifunza vitu vingi kwa sababu inahusisha kolabo kubwa na mipango mikubwa.

"Mimi napenda kuwapa nafasi Producers wenzangu haswa wachanga, napenda wafike sehemu kubwa so as long as tuna sound nyingi na watu hulalamika tunashindwa kuwafikia wasanii wakubwa;

'So mimi natoa nafasi na kupitia mimi producers wengine wanaweza wakapata nafasi ya kufanya naye kazi (Diamond) huenda nyimbo zao zikasikika mwisho wa siku wote tunataka muziki wetu ufike mbali zaidi, naweza nikawa kitu sina mimi, akawa macho Mwingine, hivyo album ikiwa na sound nyingi na tofauti ndio itafanya muziki wetu uwe mkubwa zaidi.

"Diamond ni msanii mkubwa sana na msanii wa kimataifa ni moja kati ya icon ambazo tunazo kwa hiyo mtu ambaye anatuwakilisha vizuri nje, ni vyema tukamtumia yeye mwenyewe kufikisha muziki wetu mbali kwa upande wa producers''.

S2kizzy ni mtayarishaji ambaye ameshafanya kazi kadhaa zilizomshirikisha Diamond kama Tetema aliyofanya na Rannyvan, pia amefanya kazi na wasanii wengi wakiwemo Jux, Vanessa Mdee, Rannyvan, Harmonize, Whozu na wengine kibao.

No comments