BUMBULI AITISHA TANZANIA PRISONS, KUHUSU ASUKILE

Anaandika Hassan Bumbuli, Msemaji wa Yanga katika ukurasa wake wa Facebook:
"Nahodha wa
Tanzania Prisons Benjamin Asukile ametoa tuhuma mzito dhidi ya Yanga, 1.
Amesema tuliwazidi kwa sababu tulimuongeza Refa upande wetu, Hili tunataka alithibitishe, Kivipi na kwa
namna gani!?
2. Walikuwa
wakiwapigia simu na kutaka kutoa Mil 40 (Rushwa) I'll watuachie game, hili pia
tunataka alithibishe mbele ya ya Mamlaka husika.
Hakuna namna ambayo
Yanga tunaweza kuvumilia kuchafuliwa kwa
kiwango hiki. Asukile anasahahu kwamba
ushindi pekee ambao Timu yake imewahi kuupata tangu msimu wa 2018/19 hadi sasa
ni sare tatu tu katika mechi Nane.
Msimu wa 2018/19
tuliwafunga mabao 3-1 kwao, pia tukawafunga 2-1 kwa Mkapa. Msimu wa 2019/20
tuliwafunga 1-0 kwao (Samora), wakaambulia sare kwa Mkapa na tukawatoa kwenye
FA kwa mabao 2-0.
Msimu huu
wamebahatika kupata sare mechi zote mbili za Ligi, na Jana wamekaa kwao, sasa
huo ujasili wa Asukile na kujitoa ufahamu kuona wao ni wababe ameutoa
wapi? Tutazifikisha tuhuma hizi zote kwa
Mamlaka husika ASAP.

Post a Comment