TUMEPEWA AKILI ZA KUFIKIRI, SI KUTISHANA- RC MTAKA

 

Mjue Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka | Gazeti la Jamhuri

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Antony Mtaka akiwa katika vikao vya kuanisha vipaumbele mkoani , amesema yeye hayupo pale kutisha na kumtishia mtu bali yupo pale kwa ajili ya kuunganisha akili za watu waliozajaliwa ili kuleta matokeo mazuri mkoani humo.

RC Mtaka, amesema watumishi wa wilaya zote Dodoma wachague vipaumbele vichache, hawana haja ya kuwa na vipaumbele vingi.

Akitolea mfano kwa wilaya ya Kongwa kwa Job Ndugai, Mheshimiwa Mtaka amesema Kongwa kuna ng'ombe wengi sana, lakini Je kipaumbele kiwe nyama au maziwa au uzalishaji wa ng'ombe zaidi?

Amesisitiza kwa wilaya ya Kongwa hakuna haja ya kushika vipaumbele vyote kwa wakati mmoja, ni kuchagua kimoja na kuunganisha akili na mawazo ili kupata manufaa.

RC Mtaka amesisitiza vipaumbele vikiwa vingi sana vinatutoa kwenye mstari na baadae tunapata matokeo mabaya

RC Mtaka amesisitiza anapenda astaafu kazi kwa heshima na hata watu wakimuona waweze kumsalimia na kucheka pamoja, Amesisitiza watu inabidi waone fahari kuwaona viongozi wao Dodoma.

Aidha maeneo ambayo wanalima alizeti RC Mtaka amesema suala sio kulima alizeti tu, suala ni kujua katika alizeti kipaumbele ni mafuta au alizeti yenyewe? 

RC Mtaka ameeleza kuwa ni muhimu kuzalisha kwa kuangalia soko lipo wapi? Ni soko la ndani au la nje, na Je kuna uhitaji wa hilo zao sokoni.

RC Mtaka amesisitiza kuwa RC Mahenge anayeondoka Dodoma alikuwa mtu mpole na mnyenyekevu sana na hakuwa na walinzi kwenye mambo yake nje ya ofisi kwani aliishi maisha ya kuheshimu watu.

RC Mtaka amesisitiza anapenda siku akifikisha umri wa RC Mahenge na yeye awe mtu humble na mcheshi sana.

Akihoji kama RC Mahenge alikuwa anatembea bila ulinzi, kwanini Mkuu wa wilaya ujaze walinzi?

No comments