MISS TANZANIA AANGUKIA PUA URITHI WA DK. MENGI



MISS Tanzania 2000, Jaqueline Ntuyabaliwe ambaye aliolewa na mfanyabiashara maarufu nchini, Dk. Reginald Mengi mwaka 2011, ameangukia pua mahakamani baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania Masijala ya Dar es Salaamkuamua kuwa mtoto wa Marehemu Reginald Mengi;-Abdiel na kaka wa marehemu, Benjamin Mengi kuwa wasimamizi wa mirathi ya mali alizoacha marehemu (Reginald Mengi). Katika uamuzi huo, mahakama imeagiza usimamizi na mgawanyo wa mirathi uanze mara moja.

Katika shauri hilo watoto wa marehemu Dkt. Mengi walikuwa wakipinga wosia uliodaiwa kuachwa na Marehemu baba yao kwa madai kwamba wosia huo haukufungwa ‘sealed’ na saini iliyopo kwenye wosia huo ni tofauti na sahihi zingine za Marehemu na pia kwa wakati huo baba yao hakuwa na uwezo wa kuandika kutokana na matatizo makubwa ya kiafya aliyokuwa nayo tangu mwaka 2016.

Aidha watoto hao walidai kuwa wosia uliwabagua na urithi wote aliachiwa mkewe mpya na watoto mapacha na hivyo wosia huo ulikuwa kinyume na sheria sababu uliwabagua watoto bila sababu za msingi na za kisheria.

No comments