TANZANIA, BRAZIL KUSHIRIKIANA KIMICHEZO
WAKATI ikifahamika kuwa taifa la Brazil ni mahiri katika soka duniani, jambo la kufurahisha ni kuwa nchi hiyo sasa imekubali kushirikiana na Tanzania ili kuangalia namna ya kufanya programu ya kubadilishana wakufunzi.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa
na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa amesema Nchi ya Brazil ipo tayari
kushirikiana kitaalamu na Tanzania kati Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya kilichopo
Jijini Mwanza kwa kufanya Programu ya kubadilishana Wakufunzi wa michezo.
Bashungwa alisema jana Mei 21, 2021Jijini Dar es Salaam
alipokutana na Balozi wa nchi hiyo Antonio Augusto Martins Cesar ambapo amemuomba
kuialika timu ya Taifa ya Wanawake ya
nchi hiyo kuja kucheza na Tanzania ili kuleta motisha ya kukuza Michezo ya
wanawake ikiwa ni sehemu ya kutimiza maagizo aliyoyatoa Rais Samia Suluhu
Hassan hivi karibuni.
Naye Balozi huyo amemshukuru Waziri Bashungwa kwa kupata muda
wa kuonana nae ambapo amepokea maombi ya ushirikiano baina ya Brazil na Tanzania
Katika sekta ya Michezo na kuahidi kuwasiliana na serikali yake mapema
iwezekanavyo ili kujua ni jinsi gani wanaweza kufanya mabadilishano ya
wakufunzi wa michezo na pia kukaa na Idara ya Michezo kuainisha ni namna gani
wanaweza kukisaidia Chuo cha Maendeleo ya Michezo Nchini. Aidha , Balozi huyo
ameridhia kuialika timu ya Taifa ya Wanawake ya nakuahidi kulifayia kazi suala
hilo.

Post a Comment