'STRESS' ZINAKUTOAJE KWENYE RELI?

HAPA duniani bwana mambo ni mengi kweli kweli, kiasi kwamba kuna vitu vinaendelea hadi ukiwa peke yako unajiuliza, hivi hili limetokeaje, maana hata huamini.
Sisi waswahili
wakati mwingine mtu akiishi miaka 80 na kuendelea huko, inabidi umpongeze sana,
maana hapa katikati amepitia misukosuko mingi sana, kuanzia nyumbani, kazini,
barabarani, vijiweni na hata katika mitikasi mingine nje ya kazi tunazozifanya.
Unaweza ukawa
umetoka zako home fresh kabisa, unaenda zako kazini, uwe kwenye usafiri wako
binafsi, upande bajaj, bodaboda au hata daladala. Chukulia umepanda daladala
kwa mfano, unasubiri abiria wajae.
Mara mpiga debe
anakuja upande uliokaa, halafu analipiga gari kwa nguvu eti anaitia abiria.
Kwanza anakushtua, halafu anakupigia kelele, unaweza kupandisha hasira ghafla
na kujikuta anaanza kutupiana naye maneno. Ni bora awe mstaarabu akuelewe
kwamba kitendo alichofanya siyo cha kiungwana, tatizo linakuja pale anapoamua
naye kuja juu halafu anakupa maneno ya kuudhi.
Hapo ikishakuwa
hivyo, inakubidi tena ujitafakari na uamue unyamaze tu, maana vinginevyo
unaweza kuamua kushuka ukabiliane naye. Sasa hapo kwenye kukabiliana naye ndipo
panapotisha, maana hujui nini kitatokea. Unaweza kumpiga ukashinda, lakini
umemuumizaje? Anaweza kukupiga ukashindwa, umeumiaje?
Kwa vyovyote,
uamuzi wa kukabiliana naye ni hatari zaidi kwako kuliko kwake kwa sababu wewe
ndiye utaharibikiwa na mambo yako mengi muhimu kuliko yeye. Kama utakuwa
umemuumiza au kinyume chake, suala hilo linaenda polisi na si unajua, wale
ndugu zetu hawana jambo dogo maana kwanza wote mnakuwa mmevunja sheria ya
kupigana hadharani.
Halafu mmeumizana.
Ni lazima fedha itahusika. Asikudanganye mtu, huwezi timiza jambo lako polisi
bila hela, labda uwe na mkubwa anakusimamia, vinginevyo hata ukiwa na ndugu
yako, atakushawishi 'umtoe' afande maana ndiye kawezesha hilo jambo liishe!
Huo ni mfano mmoja
tu kati ya changamoto nyingi tunazokutana nazo barabarani. Wengine
wanazinguliwa na bodaboda, wengine bajaj, wengine madereva teksi na wengine
madereva wa daladala. Si unakumbukaga kisa cha mkuu mmoja wa mkoa aliyewahi
kumpiga risasi na kumuua dereva wa daladala baada ya 'kulipiga pasi' Prado
lake?
Hizi changamoto za
barabarani ni cha mtoto, kuna watu wana changamoto majumbani mwao, kunawaka
moto. Baba na Mama hawapikiki chungu kimoja, familia imesambaratika na
umasikini unawanyemelea.
Usimuone mtu
anatembea anaongea peke yake barabarani, ukute hapo anamfokea mtu, anamtukana
bosi wake kazini au hata anamkaba mtu shingo.
Kuna watu huko
makazini kwao wanaandamwa sana na mabosi, ana anapigwa vita sana na wenzake,
kiasi kwamba kibarua chake wakati wowote kitaota nyasi. Hana raha. Au wengine
ndiyo hivyo, wamepewa barua za kuachishwa kazi.
Yaani hata kosa
lako hulijui, unaambiwa kazi basi. Hapo jana tu ndiyo umetoka kusambaza pesa za
mkopo uliokopa ili ufanyie mambo yako urejeshe taratibu kwa taasisi hizi za
mikopo. Lazima tumbo likuume!
Kwa kifupi,
namaanisha zipo changamoto nyingi na za aina tofauti. Usije ukamuona mtu ana
jumba kubwa, gari la thamani na watoto wote English Medium Schools ukadhani
jamaa yupo comfortable!
Huwezi jua kilicho
nyuma yake, wengine wamesuswa na familia zao. Yaani pamoja na pesa zake, lakini
hana uhusiano kabisa na wazazi wake, ndugu zake wa kuzaliwa pamoja na hata
ukoo. Anaishi kama mnyama ambaye ana mashaka ya kulogwa wakati wowote. Huyo,
akiona ndege katua kwenye paa lake, akili yote anaipeleka kwa uchawi,
anakimbilia kwa mganga.
Lakini, pamoja na
yote, hizi changamoto ambazo tunapenda kuita wakati mwingine msongo wa mawazo
au stress, tunazikaribisha sisi wenyewe. Laiti kama ungejua, hicho kitu
kiuhalisia hakipo!
Believe me, adui
yako namba moja ni wewe mwenyewe. Kwa nini, kwa sababu ni wewe ndiye unayeanza
kuutengeneza wasiwasi akilini mwako, ukiamini kuwa jambo lililokukuta ni baya
na litakusumbua. Niliwahi kukoma kitabu kimoja na ningekushauri ikikufaa
kitafute, kinaitwa How To Start Living Again.
Hiki ni kitabu
kinachokurudisha katika maisha baada ya kupatwa na kile kinachokutesa. Listen,
hakuna jambo geni hapa duniani ambalo wewe utakuwa mtu wa kwanza kulifanya au
kufanyiwa, hakuna. Kama lipo hebu jikumbushe mwenyewe kwamba hili hukupata
kulisikia.
Kuna watu wanajiua
baada ya kufukuzwa kazi..Came on, wewe vipi? Mbona unafanya ujinga namna hii?
Halafu anaacha ujumbe kuwa nimejiua kwa sababu nina madeni na kazi nimefukuzwa,
shit!
Kuna watu wanadaiwa
billions of money na wamefilisika, lakini bado wanadunda tu. Kama Mungu
alikujaalia ukafanikiwa kujenga kibanda, ukachukulia mkopo ukashindwa kulipa
afu wanaokudai wakaja kukichukua, usijali. Hiyo ndiyo mipango ya Mungu, ana
kusudi lake!
Uliwezaje kupata
hela ya kukijenga mara ya kwanza ushindwe mara ya pili? Eti umefumaniwa na
mtoto wa ndugu yako ukiwa umelala naye, sasa unaamua kujiua eti unakwepa aibu.
Ha ha haaaa, hebu acha kutuchekesha, unaona aibu?
Kama ulikuwa na
aibu ungetafakari mapema kabla ya kuamua kumuingia na hivyo ungejiepusha nayo,
lakini kwa vile uliamua liwalo na liwe, means ulikuwa umejiandaa kisaikolojia.
Komaa, pambana na aibu hiyo mbele yako kwa sababu wewe siyo mtu wa kwanza
kufumaniwa ukiwa umelala na mtoto wa ndugu yako.
Kuna watu
walifumaniwa na watoto wao wa kuwazaa na bado maisha yanaendelea. Hapa
simaanishi kwa mifano hii miwili nakushauri ukopee fedha kibanda chako au
umtongoze au kulala na mtoto wa ndugu yako. Nimetoa mifano hii kwa sababu ndiyo
inayoeleweka mapema.
Maana yangu ni kuwa
ili kukabiliana na matatizo makubwa, unapaswa kujiuliza kama wewe ni wa kwanza
kuyapata au kama unadhani utakuwa wa mwisho. Kwa vyovyote jibu litakuwa HAPANA.
So, kabiliana nalo kwa namna yoyote.
Kuna mtu yupo
sehemu anaweza kukusaidia, hata kama siyo kwa asilimia kubwa. Kitu cha kwanza
unachopaswa kufanya ni kumshirikisha mtu unayemuamini katika tatizo lako. Ni
mtu gani unayemuamini?
Hii pia inaweza kuwa
changamoto, lakini kifupi ni yeyote ambaye unaamini ataguswa na
utakachomweleza, siyo lazima awe rafiki yako wa miaka mingi. Mtu mwingine
anaweza kuwa ni mkubwa au mdogo kwako na hamjawahi kuwa na ukaribu wa kutisha,
lakini anaonekana ni mtu mwenye uelewa, MFUATE.
Huyu kwa vyovyote
atakushauri uvute kwanza subira. Na hiki ndicho kitu kikubwa unachokihitaji,
SUBIRA. Unakaaje na mawazo ya kukosa ajira hadi unachanganyikiwa wakati kuna
kazi kedekede mjini hapa? Mbona kuna watu kama wewe wanabeba mchanga, wanaponda
kokoto na wanaishi na familia zao. Mbona kuna wengine ni mama ntilie na
wanasomesha watoto wao?
Stress ni ugonjwa wa kujitakia, ukatae...

Post a Comment