SIYO DILUNGA, NI MUDATHIRI YAHYA WA AZAM

SHIRIKISHO la Soka Nchini, TFF limesema
kiungo wa Klabu ya Simba, Hassan Dilunga ameandikwa kimakosa katika kikosi cha
timu ya taifa kilichoitwa siku ya leo kujiandaa na mchezo wa kirafiki dhidi ya
Malawi.
TFF imesema Dilunga hajaitwa na aliyeitwa ni Mudathiri Yahya
wa Azam FC.

Post a Comment