KAZI IMEANZA, JAMBAZI MMOJA AUAWA DAR

IKIWA ni siku moja tu baada ya Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makala kuagiza Jeshi la Polisi kuwanyang'anya
majambazi silaha kabla hawajazitumia, Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es
Salaam limefanikiwa kumuua Jambazi mmoja aitwae Kilambo Obale maarufu Nyasairo
(44) mkazi wa Chanika.
Kamanda Camilius Wambura amesema
Mtuhumiwa huyo alikamatwa May 27,2021 saa 5 usiku kwa makosa ya kujihusisha na
ujambazi Mkoa wa Mara na Dar es salaam.
Baada ya Mtuhumiwa kuhojiwa alikiri kujihusisha na matukio
hayo na anamiliki silaha hivyo Askari walimwamuru kwenda kuonesha silaha hiyo
ilipo na wakati walipofika eneo alipoifukia na kuanza kuchimba Mtuhumiwa alikurupuka
na kukimbia kuingia kwenye maporomoko ya kingo za baharÃ.
Askari walipiga risasi hewani ili kumwonya asimame lakini
hakutii na kuendelea kukimbia ambapo Askari walimpiga risasi ya mguu wa kulia
kuanguka chini na baadae kufariki akipelekwa Hospitali ya Mwananyamala.

Post a Comment