SIMBA 4G KWA MADIBA

 Simba S.C. - Wikipedia

 

Simba S.C. - Wikipedia

WAKATI mashabiki na wapenzi wa soka Tanzania wakiamini mwakilishi wa nchi katika Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Simba ya Tanzania  itaibuka na ushindi katika mchezo  wake wa kwanza wa robo fainali dhidi ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusiini leo, wekundu hao wa Msimbazi, wamechezsea kichapo cha mabao 4-0.

Licha ya kucheza soka lao safi la kutandaza kandanda uwanjani, mabingwa hao mara tatu wa Ligi Kuu Tanzania Bara, walikosa mbinu za kuzuia mashambulizi ya kushtukiza dhidi ya timu hiyo, inayoshika nafasi ya tisa katika msimamo wa Ligi Kuu nchini Afrika Kusinii.

Kwa matokeo hayo, Simba inatakiwa kuipiga Kaizer Chiefs mabao matano kama inafikiria kuchezo nusu fainali za Africa's Champions League msimu huu.

Walichekelea sare ya watani wao Ruangwa, wao wamenuna kwa kipigo 'hevi' kwa Madiba. Hata hivyo, tofauti na WANANCHI, WEKUNDU WA MSIMBAZI wanaweza kupindua matokeo katika mchezo wa marudiano. Kumbuka, mwaka 1979, walipigwa 4-0 nyumbani Dar es Salaam na Mufulila Wonderes ya Zambia,  lakini wakaenda kumpiga 5-0 jijini Lusaka. Katika soka, nothing is impossible.   

NB Tunaomba radhi kwa kusema timu iliyoifunga Simba mwaka 1979 kuwa ni Nkana, ukweli ni kwamba timu hiyo ni Mufulila Wonderes.

 

No comments