RUBANI ALIYETOROSHA NDEGE YA TANZANIA AFARIKI


ATC.jpg

RUBANI Mstaafu wa Tanzania, kampteni Narzis Mapunda amefariki dunia jana jijini Dar es Salaam.


Mwaka 2019 Kapteni Mapunda ambae ni rubani mstaafu alitunukiwa tuzo na Rais John Magufuli kwa uzalendo wa kutorosha ndege ya Tanzania baada ya kuvunjika iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1977.

Kwa mujibu wa maelezo ya Mapunda, siku ilipotangazwa kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki imevunjika, alikuwa zamu na rating yake ya kazi siku hiyo ilikuwa kurusha ndege kutoka Nairobi kwenda Mombasa, halafu Tanga na mwisho Dar es salaam. Alipofika Mombasa, taarifa zilimfikia kwamba jumuiya imevunjika hivyo ameagizwa awashushe abiria wote Mombasa, kisha airudishe ndege hiyo Nairobi.

Ndege hiyo ilikuwa aina ya Fokker Friendship F27 anaeleza alikataa kushusha abiria kwa sababu abiria wengi kwenye ndege hiyo walikuwa wanakwenda Dar es salaam, akawaomba wamuongezee mafuta ya kumfikisha Dar na kuahidi kwamba akishawafikisha atairejesha ndege Nairobi hata hivyo wahusika walikataa kumpa mafuta kwa kigezo kuwa mafuta ya ndege yameisha.

Ndipo alipopiga hesabu yake na kuona kwamba mafuta aliyokuwa nayo yalimtosha kufika Tanga. Akaendelea na safari yake hadi Tanga na alipofika Tanga aliongeza mafuta na kwenda Dar na mara baada ya kufika alishusha abiria wote aliyokuwa nao na kuikabidhi ndege kwa wahusika pale uwanja wa ndege wa Dar es salaam - terminal 1.


No comments