ASIMULIA ALIVYOKUTANA NA USHIRIKINA SITE

JAMAA mmoja Mtanzania, ambaye alilelewa katika mazingira ya
dini tangu utoto wake, anasimulia jinsi alivyoacha kazi na kuamua kujiingiza
katika kujiajiri kwenye machimbo na vitu alivyokutana navyo.
Simulizi hii ni credit kwa Jamii Forum:
"Kwanza nitajikita kwenye mada kutokana na personal
experience ya hapa home Tz. Binafsi nimekulia mazingira ya dini sana, kwa hiyo
mambo ya uchawi au ku-practice masuala ya kiganga /jadi sikuwahi.
"Lakini kwa uzoefu na namna nilivyoona katika kutembea
mikoa ya hapa Tanzania, hasa huko vijijini watu wamelazimika kutofanya
Maendeleo, kuyahama makazi yao kwa kuogopa kulogwa. Unakuta eti Kijijini mtu
alikuwa hawezi kujenga nyumba nzuri na kuezeka bati, ukifanya hiyo kitu unaanza
kuandamwa na mambo mengine kama hayo.
Personal Experience.
"Nilipoamua ku-resign kazi na kuanza mishe zangu
binafsi, niliingia kwenye kazi za mining na huku ndio nilikutana na hayo mambo.
"Tulienda kuanzisha mining site Handeni- Tanga. Aisee,
nilikuwa nausikia tu ushirikina sasa kule ndio nilienda kuona. Yaani mtu
analoga machine (Excavator) inakuwa haifanyi chochote, tunaita mafundi wa kila
aina wanachokonoa wee ila waapi, na machine bado mpya.
"Baadae one of the labors niliokuwa nao pale site
akaniita na wenzake pembeni, wakaniambia ndugu yetu, hapa kutakuwa na kitu
kimefanyika, wakanitaka twende na mganga ili tuka unlock. Mimi nikawa siamini
kama mashine inaweza logwa na sikuwa na imani na zile mambo kabisa.
Basi nikawauliza kama wanaweza kwenda wenyewe wafanye kwa
niaba, wakasema poa niwape elfu 20 wanunue kuku, basi mshikaji akanambia
tuwape. Mini nikawapa wakaondoka bwana, hapo tumehangaika na fundi wiring na
hydrologic system wote wanasema hawaona tatizo, ila machine haina kabisa nguvu
ya kuchimba.
"Wale wadau walirudi time za jioni kama saa kumi na moja
hivi, na maji yenye dawa kwenye chupa pamoja na vimiti viwili. Wakasema
Operator wa machine aweke mfukoni kimti kimoja na kingine aweke chini ya seat
yake, na yale maji ya dawa imwagiwe machine na kuzunguka eneo la mgodi.
Operator akasema fresh ,yeye alikuwa anaamini sana, wale jamaa wakamwaga maji
kwenye machine nakuzunguka pale site, na mwingine akaenda akaleta ka kuku
kadogo akachimba shimbo pembezoni mwa site akakafukia kale kakuku kakiwa kazima.
"Baada ya hapo wakamwambia Operator awashe machine . Mi
naangalia tuu kama movie, aisee huwezi amini, machine ikawa na power kuzidi
hata uwezo wake siku zote. Nikashangaa sana, jamaa wale wenyeji wanacheka
wananiambia "karibu Tanga mgosi".
"Hii ni kwa ufupi tuu, nina mengi sana nime experience
sehemu mbali mbali hasa katika kazi ya mining, maana mnaenda kuanzisha kazi
sehem porini kumbe palikua ni mahali pa matambiko, basi vituko ni vingi
nikijaaliwa muda nitakuja andika matukio mengine . Watu wana uwezo wa kupoteza
madini aridhini, yaani unachimba wee na kuunguza hela ila huoni kitu, wakati
mwanzo mambo yalikua fresh kabisa. Lakini mwisho wa siku nina Imani na Mungu ,
hatutakiwi kuweka Imani kwa waganga kwa sababu nao ni binadamu, uchawi upo na
Mungu yupo.
"Serikali haiamini katika uchawi, ni sawa kabisa lakini
ukweli ni kwamba uchawi umelostisha sana watu, pengine watu wangekuwa na
maendeleo sehemu mbali mbali isingekuwa haya mambo. Siku hizi kidogo yanapungua
,nadhani muingiliano wa wageni na wenyeji sehemu mbalimbali unafanya watu
ku-focus kwenye maendeleo. I'm not sure kama tumeshawahi kuwa na sheria
inayokemea haya mambo kwa kuwa ni invisible world."
Naomba niishie hapo kwa leo, najua wengi wetu tuna experience
tofauti tofauti, kuwa huru ku share nasi tujifunze kitu.

Post a Comment